Friday, April 29, 2011

TAWLA Waunda Jukwaa La Jinsia Kuhusu Katiba

Mwenyekiti wa Chama Cha Wanasheria Wanawake Maria Kashonda (katikati) akisoma taarifa kwa waandishi wa habari leo Idara ya Habari Maelezo kuhusu jukwaa la kijinsia la katiba, Gender Forum Constitution  Review (GFCR) jukwaa ambalo limeundwa na TAWLA kwa kushirikiana naAsasi zisizo za Kiserikali (NGO's). Akielezea malengo ya kuundwa kwa jukwaa hilo alisema kuwa  lengo ni kutoa msukumo na msisitizo kwa Serikali kushirikisha makundi ya kijinsia  hususani wanawake katika mchakato wa kupatikana  kwa katiba mpya. Wengine ni Magdalena Kamugisha (Kushoto) ambaye ni mweneykiti wa (GFCR) na kulia ni Bi Victoria Mandari.

Waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini mwenyekiti wa chama cha wanasheria wanawake TAWLA Bi. Maria Kasonda leo Idara ya Habari Maelezo.(Picha;Mjengwablog)

No comments:

Post a Comment