Friday, April 29, 2011

Tukutane Daispora DC Mwezi Wa Kumi

Watanzania: Seattle, WA  na  Portland, OR

Kwa niaba ya Mwenyekiti  TANZASEATTLE nawakumbusha kuwa sherehe zetu za Muungano ni Jumamosi
hii tar. 30/4/2011 katika ukumbi wa Eritrean Association Hall (1528 Valentine
Place South, Seattle, WA, 98144). Sherehe zitaanza saa kumi jioni.

Kiingilio ni dola 15 (utapata chakula, utaburudika kwa fashion show, utapata
burudani ya ngoma, utacheza muziki mpaka majogoo). Vinywaji vitauzwa ukumbini (maji na soda ni dola moja moja, bia dola 3). Tutapokea cash au check tu.

Niwakumbushe tu kuwa Fashion show itaongozwa na dada ASIA IDOROUS- KHAMSIN
kutoka Taxes, Ngoma na  Mr. Kedmon Mapana (Jiandae kucheza ngoma, usisahau khanga za kujifunga) , Muziki na DJ Dully).

Tafadhali usikose, alika jamaa  na marafiki (wageni wote watalipa kiingilio kama
kawaida)
=================   NJOO TUSELEBUKE

No comments:

Post a Comment